Posts

001 - Mtakatifu, Mtakatifu,Mtakatifu "Holy, Holy, Holy"

 001 - Mtakatifu, Mtakatifu,Mtakatifu "Holy, Holy, Holy" 1 U Mtakatifu! Mungu mwenyezi! Alfajiri sifa zako tutaimba; U Mtakatifu , Bwana wa huruma, Mungu wa vyote hata milele. 2 U Mtakatifu! Na malaika Wengi sana wanakuabudu wote; Elfu na maelfu wanakusujudu Wa zamani na hata milele. 3 U Mtakatifu! Ingawa giza Lakuficha fahari tusiione, U Mtakatifu! Wewe peke yako, Kamili kwa uwezo na pendo.

002 - Twamsifu Mungu "We Praise Thee, O God"

 002 - Twamsifu Mungu "We Praise Thee, O God" 1 Twamsifu Mungu, Mwana wa upendo Aliyetufia na kupaa juu. Chorus Aleluya! Usifiwe, Aleluya! Amin; Aleluya! Usifiwe, utabariki. 2 Twamsifu Mungu, Roho mtakatifu, Akatufunulia Mwokozi wetu. 3 Twamsifu Mwana, aliyetufia Ametukomboa na kutuongoza. 4 Twamsifu Mungu wa neema yote Aliyetwaa dhambi, akazifuta. 5 Twamshe tena, tujaze na pendo. Moyoni uwashe moto wa Roho.

003 - Mungu Atukuzwe "To God Be The Glory"

 003 - Mungu Atukuzwe "To God Be The Glory" 1 Mungu atukuzwe kwa mambo makuu,  Upendo wake ulitupa Yesu, Aliyejitoa maisha yake, Tuwe nao uzima wamilele. Chorus Msifu, msifu, dunia sikia; Msifu, msifu, watu wafurahi; Na uje kwa Baba, kwa yesu Mwana, Ukamtutukuze kwa mambo yote. 2 Wokovu kamili, zawadi kwetu, Ahadi ya Mungu kwa ulimwengu; Wanaomwamini na kuungama, Mara moja wale husamehewa 3 Alitufundisha mambo makuu,  Alihakikisha wokovu wetu, Lakini zaidi, ajabu kubwa, Yesu atakuja na tutamwona.

004 - Jina LA Yesu Salamu "All Hail The Power"

 004 - Jina LA Yesu Salamu "All Hail The Power" 1 Jina la Yesu, salamu! Lisujidieni, Ninyi mbinguni, hukumu, Na enzi mpeni Ninyi mbinguni, hukumu, Na enzi mpeni 2 Enzi na apewe kwenu, watetea dini; Mkuzeni Bwana wenu, Na enzi mpeni Mkuzeni Bwana wenu, Na enzi mpeni 3 Enyi mbegu ya rehema nanyi msifu; Mmeponywa kwa neema, Na enzi mpeni Mmeponywa kwa neema, Na enzi mpeni 4 Wenye dhambi kumbukeni ya msalabani Kwa furaha msifuni, Na enzi mpeni Kwa furaha msifuni, Na enzi mpeni. 5 Kila mtu duniani msujudieni Kote-kote msifuni, Na enzi mpeni Kote-kote msifuni, Na enzi mpeni. 6 Sisi na wao pamoja tu mumo sifani. Milele sifa ni moja, na `mpeni` Milele sifa ni moja, na `enzi mpeni`

005 - Na Tumwabudu Mfalme Mtukufu "O Worship The King"

 005 - Na Tumwabudu Mfalme Mtukufu "O Worship The King" 1 Na tumwabudu  huyu Mfalme, Sifa za nguvu zake zivume; Ni ngao, ni ngome, Yeye milele, Ndizo sifa zake kale na kale. 2 Tazameni ulimwengu huu, Ulivyoumwa, ajabu kuu; Sasa umewekwa pahali pake, Hata utimize majira yake. 3 Kwa ulinzi wako, kwetu Bwana, Twakushukuru, U mwema sana; Hupewa chakula kila kiumbe, Kila kitu kila mahali pake. 4 Wanadamu tu wanyange sana, Twakutumaini wewe, Bwana; Kamwe haupunguiwsako wema, Mkoombozi wetu, Rafiki mwema.

006 - Kumekucha Kwa Uzuri "The Morning Bright Rosy'

 006 - Kumekucha Kwa Uzuri "The Morning Bright Rosy' 1 Kumekucha kwa uzuri. Nafumbua macho; Baba amenihifadhi, Ni wake moto. 2 Bwana niwe leo kutwa Ulinzini mwako; Nisamehe dhambi, niwe Mikononi mwako. 3 Roho wako anikae moyoni daima; Anitakase, nione Uso wako.

007 - Mungu Msaada Wetu "O God Our Help In Ages"

 007 - Mungu Msaada Wetu "O God Our Help In Ages" 1 Mungu Msaada wetu tangu miaka yote; Ndiwe tumaini letu la zamani zote. 2 Kivuli cha kiti chako ndiyo ngome yetu, Watosha mkono wako ni ulinzi wetu. 3 Kwanza havijakuwako nchi na milima, Ndiwe Mungu; chini yako twakaa salama. 4 Na miaka elfu ni kama siku moja kwako; Utatulinda daima, tu wenyeji wako. 5 Bwana msaada wetu tangu miaka yote, Mlinzi wetu na ngome, daima, milele.