016 - Ninakuhitaji "Blessed Lord, How Much I Need Thee"

 016 - Ninakuhitaji

"Blessed Lord, How Much I Need Thee"



1

Bwana ninakuhitaji! Nimpofu, maskini;

Unishike mkononi, Kwako napata nguvu.


Chorus

Kila saa, kila saa Bwana ninakuhitaji;

Kila saa, kila saa, Unilinde kila saa.


2

Univike na mavazi Ya usikivu wako;

Nguo zangu ni machafu, Nazitamani zako.


3

Wewe ukiniongoza Nitakwenda salama;

Nenda nami siku zote, U nuru na uzima.


4

Na ikiwa m-beleni Sehemu yangu ngumu,

Au ikiwa furaha, Unilinde kila saa.


Comments