015 - Nena Mungu "Speak To My Soul"

 015 - Nena Mungu

"Speak To My Soul"



1

Nena rohoni Yesu, Nena kwa upole

Sema kwangu kwa pendo, "Huachwi upweke."

Fungua moyo wangu, Nisikie mara;

Jaza roho na sifa, Sifa zako Bwana.


Chorus

Kila siku unene, Vile kwa upole,

Nong`oneza kwa pole wa pendo:

"Daima utashinda, Uhuru ni wako."

Nisikie maneno; "Huachwi upweke."


2

Nena kwa wana wako, waonyeshe njia, 

Wajaze kwa furaha, Fundisha kuomba;

Wajifunze kutoa Maisha kamili,

Wahimize ufalme, Tumwone mwokozi.


3

Nena kama zamani, Ulipoitoa

Sheria takatifu: Niiweke pia;

Nipate kutukuza Wewe Mungu wangu,

Mapenzi yoko tena, Daima kusifu.


Comments